Alhamisi, 11 Julai 2013

RC IRINGA AAGIZA HALMASHAURI KUSIMAMIA FEDHA ZA MIRADI

rc 4e922
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Chistine Ishengoma akizungumza wakati wa kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC) mkoa wa Iringa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Siasa ni kilimo, Manispaa ya Iringa. (HM)

rc2 5d2f7
Wajumbe wa kikao cha RCC
  
MKUU wa mkoa  wa  Iringa  Dkt. Christine Ishengoma  ameziagiza Halmashauri  mkoa  wa  Iringa  kuhakikisha  wanasimamia  vema fedha  za miradi  zinazotolewa na serikali katika maeneo yao. Mkuu   huyo wa  mkoa  ametoa agizo hilo leo  katika  ukumbi  wa Siasa ni Kilimo   wakati  akifungua  kikao  cha kamati  ya  ushauri ya  mkoa (RCC).
Amesema kuwa  lengo la  serikali  kutuma fedha za miradi katika Halmashauri  husika ni kuwezesha kusukuma mbele  kasi ya  miradi ya maendeleo katika Halmashauri. Hivyo  alisema haitapendeza  kuona  fedha za miradi katika Halmashauri  zinakosa usimamizi mzuri na  kupelekea  miradi  kukwama  kumalizika kwa wakati.
Alitaka viongozi  wa Halmashauri kubuni miradi  ya kuziwezesha  Halmashauri  zao  kuongeza mapato  zaidi.
Alisema bila ya  Halmashauri kubuni  miradi  ya  kiuchumi uwezekano  wa Halmashauri  kujiendesha utakuwa mdogo  zaidi.
Alisema watumishi  wasiojituma katika kazi  mkuu wa mkoa  ametoa onyo kwa  watumishi hao  na kuwa kamwe  hata wavumilia. Katika  hatua  nyingine  mkuu  huyu  wa mkoa ametoa agizo kwa jeshi la polisi  mkoa  wa Iringa kupitia  askari  wake wa usalama barabarani  kuwakamata na  kuyakamata  na  kuyatoza fani  magari  yote  ya abiria ambayo yatapita katika mkoa  wa Iringa  bila kuwa na  vifaa vya  kuhifadhia  taka na  yale  yatakayobainika yakichafua mazingira  ovyo. Chanzo: Francis Godwin

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...