Jumatano, 27 Novemba 2013

WAOMBA KUJENGEWA DARAJA GAIRO


WANANCHI wa Kijiji cha Madege kata ya Chakwale wilaya   ya Gairo Mkoani Morogoro Wameiomba Serikali kuwajenga daraja la Mto Kibedia ili kuwanusuru maisha yao hususani wakati wa mvua.
 

Wananchi hao walisema hayo jana wakati  wa ziara ya viongozi wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Morogoro waliotembelea katika kijiji hicho kwa lengo la  kukagua ilani ya uchaguzi.

Mmoja wa wananchi kutoka kata hiyo ya Chakwale Mwidadi Ibarahimu alisema kuwa daraja hilo halina kivuko na kwamba wananchi wake huvuka kwa shida hali inayosababisha kila mwaka vifo kwa wanancho wanaotumia mto huo.

‘’ kutokana na kutokuwa na kivuko katika mto huu, wananchi wanapoteza maisha, unakuta maji yamejaa ghafla na watu wako ng’ambo ya pili na kwamba wanapojaribu kuvuka huzolewa na maji’’ alisema.

Hata hivyo wananchi hao wamelalamikia pia barabara ya Iyogwe inayounganisha na wilaya ya Kilindi mkoani Tanga kujengwa nyembamba ukilinganisha na ile inayokutana na ya Ngiloli  huko Kilindi.

Walisema kuwa barabara hiyo ni moja ya ahadi ya Rais wakati wa  kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010 ambapo aliwaambia imependishwa hadi na kuwa ya Tanroad   badala ya Halamshauri kama ilivyokuwa awali.
Kwa upande wake Hasan  Chobo alisema kuwa pamoja na kuwa barabara hiyo ni ya kiwango cha changalawe lakini ilipaswa ijengwe kwa viwango vinavyosatahili ikiwa ni pamoja na kuwa na mifereji ya kupitisha maji ya mvua pamoja na upana unaokidhi mahitaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...