Alhamisi, 21 Novemba 2013

CHADEMA YAWANYANYASA WANANCHI KILOMBERO


VIONGOZI wa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema katika serikali ya kitongoji cha Mgudeni kijiji cha Mkangawalo, kata ya Mngeta wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro wamelalamikiwa kuwafanyia vitendo vya unyanyasaji wananchi wa eneo hilokuwapakia katika pikipiki na  kuwafunga pingu mikono katika machuma ya pikipiki .

Wananchi hao walisema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara  wakati wa ziara ya katibu wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Morogoro Rojas Romuli uliofanyika katika kitongoji hicho cha Mgudeni

Wananchi hao walisema kuwa viongozi hao wa Chadema ambao wengi ni viongozi wa serikali ya kijiji hicho kwa kushirikiana na afisa mtendaji aitwaye Rajabu Kipolelo   wamekuwa wakiwafanyia wananchi wa eneo hilo vitendo hivyo pale mwananchi anaposhindwa kulipa faini mbalimbali kijijini hapo.

Mmoja wa wananchi ambaye aliwahi kufanyiwa unyanyasaji huo Maduka Mwela alisema kuwa yeye alitakiwa kulipia kiasi cha shilingi 300,000 kama malipo ya kodi ya ardhi na kwamba alitoa shilingi 180,000 za awali lakini cha kushangaza siku iliyofuata alikuta amewekewa alama  ya msalaba mwekundu katika shamba lake kisha kufuatwa na askari mgambo na kumkamata.

Alisema kuwa mgambo hao walimfunga mkono mmoja nyuma ya pikipiki  baada ya kumpakia na kisha kuondoka naye hadi kwa mtendaji huyo wa kijiji.
‘’ Nilipofika mtendaji huyo alinipokea kwa maneno ''nyinyi ndio mnakaa vikao  na chama chenu cha CCM halafu mnapinga kulipa ada ya ardhi'' Tulibishana kwa masaa kadhaa ‘’ Alisema

Alisema kuwa wananchi wa kijiji hicho baada ya kuona tukio hilo waliandamana hadi katika ofisi ya mtendaji huyo kushinikiza mwenzao huyo ambaye ni balozi wa CCM aachiwe na ndipo afisa huyo alipomwachia.

Kwa upande wake Richard Mwamwanga ambaye ni mjumbe katika serikali hiyo ya kijiji ya mseto alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakijipangia bei za ada kinyume na utaratibu kwa lengo la kuwakomoa wananchi.

Alisema kuwa awali wakati serikali ya kijiji hicho ilipokuwa ikiongozwa na CCM walikuwa wakilipia ardhi kiasi cha shilingi 20,000 ambapo walipoingia wao madarakani walipandisha hadi kufikia 40,000 kwa hekari.

Hata hivyo mjumbe huyo alisema kuwa mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho ambaye anatokana na chama cha Chadema Stelatoni Njaani amekuwa akiongoza kwa njia ya udikteta kutokana na kwamba maamuzi anayoamua yeye na wenzake wa Chadema hataki mtu mwingine atoe hoja ya kuhoji.

Naye Deus Makaranga, katibu wa baraza la wazee kijijini hapo alisema kuwa viongozi hao kwa kushirikiana na mtendaji huyo wamekuwa wakitoa risiti feki katika kulipia mashamba pamoja na michango mbalimbali ya maendeleo.

Alisema kuwa wamekuwa wakitumia risiti moja kuandika mchango zaidi ya mmoja sambamba na kutoa risiti  kwa watu tofauti zenye namba zinazofanana.

 Kwa upande wake Gidius Alois Mwagombeka alisema kuwa yeye alikuwa mweyekiti wa kijiji cha Mkangawalo na kwamba viongozi hao wa Chadema walimfanyia hila kwa kumtuhumu kufanya ubadhilifu wa fedha za maendeleo  katika kitongoji hicho hali iliofanya mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti ambaye alikuwa akikaimu wilaya hiyo baada ya mkuu wa wilaya hiyo  Evarist Ndikilo kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa kumwondoa madarakani.

Alisema kuwa hiyo ilikuwa mwaka 2012 na kwamba tume iliundwa katika kitongoji hicho dhidi ya tuhuma hizo na kubaini kuwa sio za kweli.

Mwisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...