Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali wakiwa katika mkutano wa siku
ya uhuru wa vyombo vya habari kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika
Jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC ambapo Mei 3
ndio kilelel cha maadhimisho hayo .
Wajumbe hao wakifutilia kwa makini mkutano huo wa aina yake .
Wakongwe katika tasnia ya habari nao walipata fulsa ya kuhudhuria mkutano huo kama wanavyoonekana katika picha.
Miongoni mwa wajumbe waliohudhuria mwenyekiti wa jukwaa la wahariri
Absalam Kibanda naye alikuwa miongoni mwao ambaye mwaka jana alipata
tunzo ya mfuko maalumu ulioanzishwa wa kuasaidia waandishi wa habari
wanaopatwa wa majanga ujulikanao kama Mwangosi
Bujaga Kadago alieyavaa kikoti cha bluu ni miongoni mwa wanataaluma
wakonge nchini ambao huwezi kuzungumzia historia ya habari nchini bila
kuwagusa
Taasisi mbailmbali zilipata fulsa ya kushirikia mkutano huo kama wanavyoonekana katika picha,
Habari zaidi soma hapa chini,
Mkurugenzi wa muungano wa clabu za waandishi wa habari nchini Abubakar
Karasani amesema mfuko wa kuasaidia waandishi wa habari nchini
ujulikanoani kama mfuko wa Mwangosi Media Fund unaandaliwa kuwa kama
taasisi maalumu ya kusaidia waandishi wa habari wanaopata majanga hapa
nchini,
Alisema mfuko huo utakuwa unalenga kutaoa huduma kwa waandishi
wanaopatwa na majanga ya kushitakiwa ambapo watasaidiwa kupatiwa msaada
wa kuwezeshwa wakati wa kesi zao.
Pia wale watakaokuwa wakipata matatizo ya kuumizwa wakiwa kazini mfuko
huo utawahudumia kwa kuwapatia matibabu pamoja na huduma zingine katika
familia zao.
Kwa wale ambao wanakuwa wapo katika mazingira hatarishi ya
kufuatwafuatwa na watu wenye nia mbaya mfuko huo utawawezesha kuwapeleka
mahali na kuwahifadhi hadi hapo usalama wao utakapoimarika.
Hata hivyo alisema mfuko huo kila mwaka unatoa tunzo kwa mwandishi bora
ambaye amepatwa na majanga ya kumizwa na kwamba tunzo hiyo ni tofauti
na zingine.
alisema tunzo hizo hutolewa sio kwa kushindwanishwa bali jopo la majaji
hukaa na kuangalia kwa makini ni mwandishi gani katika mwaka huo
amepatwa na majanga makubwa na hivyo kuweza kumpatia tunzo.
Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri Kibanda aliwatupia lawama waharirir
wenzake kwa kutokuwa na umoja pale linapotokea tatizo la mwandishi na
hivyo kuanza kuwahukumu kuwa ni wanachama wa chama fulani bila kufanya
utafiti juu ya jambo kama hilo.
alisema linapotokea janga la mwandishi wahariri hao hukaa pembeni na
kuanza kusema hivyo na kuacha kushughulikia matatizo hayo kwa nguvu ya
pamoja.
Hata hivyo katika mkutano huo wakati wa majadiliano, suala la maadili
lilichukua nafasi kubwa kwa kuwataka waandishi wa habari kujaribu
kufanya kazi kwa maadaili ili kuepuka kujidhalilisha kwa kuandika habari
zisizo sahihi na hivyo kulazimika kuomba radhi mara kwa mara.
mada mbalimbali zilitolewa katika mkutano huo ambapo mada iliokuwa na
mvuto na kupata wachangiaji wengi ni mada ya Freedom Of Expression in
the Cyberspace ( Challenges and opportunities in the Social Media)
ambapo katika mada hiyo mtoa mada Simon Berege kutoka Chuo kikuu cha
Iringa aliwataka waandishi wa habari kuwa makini na vitu wanavyoweka
katika mitandao ya kijamii kwani mara ngingi vinaweza kuwafanya wakapata
mafanikio au kupoteza mwelekeo kutokana na vitu hivyo.
akitolea mfano Berege alisema wapo waandishi wa habari ambao wamekuwa
kila wakati wapo katika mtandao na kuweka vitu wanavyofanya jambo ambalo
sio zuri sana .
'' Unakuta mtu yuko baa anaweka posti bia ya tatu, ya nne hiyo inashuka
hii inaweza kufanya hata wakati unaomba kazi sehemu kuonekana mlevi au
uko bz na mtandao na hivyo kukosa nafasi kwa njia hiyo'' alisema
Berege alisema kwa utafiti wa mwaka 2012 ulionyesha kuwa Afrika matumizi ya mtandao ni asilimia 7 huku Tanzania kwa sasa utafiti unaonyesha watumiaji ni asilimia 19.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni