MEYA MORO AAGIZA KUWEKWA MIPAKA KATIKA ENEO LA MZINGA NA ENEO LA WANANCHI LA KAUZENI ILI KUONDOA MGOGORO
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCm wilaya ya Morogoro mjini Fikiri
Juma akiongea wakati wa kikao cha kawaida cha baraza la madiwani
manispaa ya Morogoro.
Mwenyekiti huyo akisisitiza jambo kwenye kikao hicho
Wajumbe wa baraza la madiwani katika manispaa ya Morogoro wakiwa katika kikao cha kawaida cha baraza hilo juzi
Diwani wa kata ya Tungi Deogratias Mzeru akiwa na diwani mwenzake wa
jirani Maria Kiamani nje ya ukumbi wa manispaa mara baada ya kumalizika
kikao hicho.
Diwani wa kata ya Kilakala Ribon Mkali akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wake wa CCM wa matawi katika kata hiyo.
Habari zaidi Soma hapa Chini.
Meya wa manispaa ya Morogoro Amini Nondo ameagiza watendaji katika
manispaa hiyo kuweka mipaka katika eneo la kata ya Kauzeni linalopakana
na eneo la kambi ya jeshi ya Mzinga ili kuondokana na migogoro ya ardhi
iliopo sasa.
Alilazimika kusema hayo baada ya mwenyekiti wa CCM Fikiri Juma kutaka
mgogoro huo kushughulikiwa haraka ili kuepusha madhara kwa jamii hizo
mbili.
Alisema kuna kisa sababu kwa watendaji hao kuhakiki mipaka katika eneo hilo ili kuweza kuweka mipaka hiyo.
Hata hivyo aliagiza wananchi katika manispaa hiyo kufuga mifugo kwa
mujibu wa sheria na taratibu zilizopo badala ya kufuga mifugo mingi.
Awalia mwenyekiti huyo wa CCM alisema hakuna sababu kwa jeshi hilo na
raia kuwa na ugomvi kwani ni jamii inayohitaji kuishi kwa pamoja na kwa
kushirikiana.
'' wananchi hawapaswi kuwa na ugomvi na jeshi letu, na jeshi halipaswi
kuwa na ugomvi na wananchi hivyo niwaombe halmashauri mshughulikie
tatizo hilo ambalo linalalamikiwa kwa muda mrefu sasa.
Mwenyekiti huyo alisema malalamiko kwa wananchi hao dhidi ya jeshi la
mzinga ni wanadai kuwa wanajeshi hao wamekuwa na mifugo kupita kiasi
hivyo hulazimika kuingiza ng'ombe zao kwwnye mashamba ya wananchi hali
inayosababisha migogoro hiyo.
Kwa upande wake diwani wa kata hiyo Ahmed Mazola alisema kuwa wananchi
ndio walianza kuwa wakwanza kuishi katika eneo hilo ambapo badae ndipo
lilikuja jeshi hilo.
Alisema kila kukicha wanajeshi hao wamekuwa wakichukua sheria mkononi
kwa kuweka bicon bila ya utaratibu na hivyo kuvamia eneo la wananchi
hao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni