Ijumaa, 10 Mei 2013

TAMKO LA CCM MKOA WA MOROGORO KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA RUAHA JANA JIONI

  
  Ndugu wananchi Tarehe 24/4/2013  ulifanyika uchaguzi wa mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Ruaha. Vyama vilivyoweka wagombea vilikuwa CCM na CHADEMA. Hata hivyo mgombea wa Chadema alienguliwa baada ya CCM kumuewekea pingamizi kwa sababu alikuwa na mapungufu yaliyomwondolea sifa ya kuwa mgombea kwa mujibu wa sheria. Hivyo basi CCM ilitangazwa mshindi na siku hiyo hiyo Chadema wakashinda kitongoji. Wana CCM waliyapokea matokea bila vurugu na wakakubali kuwa Mwenyekiti wa Kitongoji ni  wa CHADEMA.  Tarehe 09.05.2013 ili kuwa siku ya kukabidhiwa rasmi ofisi kwa Mwenyekiti mpya wa Kijiji cha Ruaha, lakini wenzetu CHADEMA wakataa kumkubali huyo Mwenyekiti na wakaamua kuanzisha vurugu kubwa sana katika kijiji cha Ruaha na maeneo ya karibu yaliosababisha uharibifu mkubwa wa mali.Wamechoma nyumba,  wamefunga barabara na kusababisha uvunjifu mkubwa wa amnai eneo hilo. Tunalaani sana vurugu hizo zilizosababishwa na kundi la watu wenye nia mbaya na nchi hii wanaotaka kuivunja amnai tulionayo, wananchi wa morogoro na Watanzania kwa ujumla Tunavitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua mara moja kurudisha amani ili wananchi waendelee na shuguli zao za kila siku za kujiletea maendeleo. Kwa wale wote waliochochea vurugu hizo wachukuliwe hatua mara moja  na sheria ichukue mkondo wake.
Imetolewa  CCM  Morogoro
10.05.2012
.........................

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...