Jumapili, 2 Juni 2013

TASWIRA ZAIDI ZIARA YA KINANA MKOA WA CHOMBE













Na Francis Godwin, Njombe

WAKATI  kukiwa na  vugu vugu  ndani  ya  chama  cha mapinduzi (CCM) kwa baadhi ya  madiwani na wabunge kuacha kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi waliowachangua na badala yake  kufanya kazi  ya  kujihami  na wale  wanaonyemelea  majimbo na kata  zao ,katibu  mkuu  wa CCM Taifa Abdalrahman Kinana ametoa  onyo kali kwa  madiwani na  wabunge  hao  wasio  watumikia  wananchi  kuwa wasije kulalamika mbele ya  safari.

Huku  akiwapasha  wana makada  wa CCM wanaojipitisha katika majimbo ,kata na nafasi  za urais  kuwa  wanapoteza muda  wao bure kwani muda wa kampeni  bado na  kuwa kufanya  kampeni kabla ya muda ndani ya CCM ni kosa na pale itakapobainika wataenguliwa katika nafasi ya ugombea kutokana na kukosa  sifa na kukiuka  taratibu  za chama.

Kinana  alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na   wana CCM na  wananchi  katika mkutano  wa hadhara  uliofanyika katika kijiji  cha Rudunga wilaya ya  Wanging'ombe mkoni  Njombe .

Alisema  kuwa  kazi  kubwa waliyopewa  madiwani na  wabunge ni  kusimamia  utekelezaji  wa ilani ya CCM pamoja na  kuwawakilisha  vema  wananchi na iwapo  viongozi hao  watajikita  zaidi katika  kuendelea  kutetea nafasi  zao  bila  kuwatumikia wananchi  waliowachagua basi  watakuwa hawatoshi kuendelea kushika nafasi  hiyo.

" Madiwani na  wabunge huu ni wakati  wao  wa kuwatumikia wananchi  waliowachagua  si wakati  wa  kuendelea  kujipanga kwa  uchaguzi  mkuu  wa mwaka 2015 ambapo muda  bado haujafika  wa kuanza kampeni....pia nawaombeni kampeni zenu ziwe  za kuwatumikia  vema  wananchi ili muda ukifika  wananchi  waweze  kukuchagua kwa kazi  nzuri  uliyoifanya na si kwa kazi ya kutafuta utukufu badala ya utumishi"

Aidha  Kinana alisema  kuwa CCM hakitafanya kosa ya  kuwapoteza  wabunge  wake  wazuri ambao  wamekuwa  wakifanya kazi  zinazoonekana kwa wananchi katika majimbo pamoja na madiwani  wanaokubalika kwa wananchi kwa  kazi  zao.

Huku akisisitiza  suala la wale  wote  waliochaguliwa na  wananchi na  kupewa nafasi ya  kusimamia ilani ya CCM kuepuka  kufanya kazi kwa misingi ya  kutafuta  heshima badala ya  kuwatumikia  wananchi waliomchagua.

"Nawahakikishia  wana  CCM na  wananchi kuwa  hatutafanya kosa katika  kuwateulia wana CCM  wanaokubalika na  wale ambao  hawakubaliki kwenu na kwetu  pia hatutawakubali kamwe"

Hata  hivyo  Kinana aliwataka  viongozi  wa CCM wakiwemo wabunge na madiwani kurudisha mrejesho kwa wananchi  wao  juu ya kazi  waliyoifanya na kusimamia na kutekeleza ilani ya  CCM na pale ambapo wameshindwa  kutekeleza wasiogope  kuwaeleza  ukweli  sababu za kushindwa na kudai kuwa CCM si chama  cha miujiza ambacho  kinauwezo  wa kutekeleza kila jambo kwa  wakati.

Wakati  huo  huo Kinana  amewachangia  kiasi cha  shilingi  milioni  10 vijana  wa  kijiji   cha Mlangali kata ya Ruduga  wilaya ya  Wanging'ombe  kwa ajili ya  kuwawezesha  kuanzisha chama  cha ushirika  cha kuweka na kukopa (SACCOS) ili  kuwasaidia  kukopeshana  fedha  za miradi ya kimaendeleo.

Kinana  alisema lengo la  kuwasaidia  fedha  hizo ni kutokana na kufurahishwa na jitihada  mbali mbali za uzalishaji maji zinazofanywa na  vijana  wa kijiji  hicho kupitia mradi wa umwagiliaji uliopo katika eneo hilo na hivyo  fedha  hizo  zitawawezesha  kupiga hatua  zaidi na  kuwasaidia  wenzao  wasio na mitaji  kujiunga  katika kikundi  hicho na kukopeshwa kwa taratibu  watakazoona  zinafaa.

Pia  aliwaahidi  mizinga  ya nyuki 25 wanachama wa jumuiya ya  wazazi kijiji  cha Mlangali ili kuendeleza shughuli ya ufugaji wa nyuki na  kuchangia mifuko 20 ya  saruji kwa ajili ya umaliziaji  wa ofisi ya CCM kijiji cha Mlangali

Katika  ziara  hiyo wilaya ya  Wanging'ombe  jumla  ya  wanachama  zaidi ya 100 kutoka vyama  vya upinzani kikiwemo Chadema, CUF, TLP na  wengine  wasiokuwa na chama walijiunga na CCM wakiwemo waliokuwa  viongozi wa Chadema wilaya  hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...