Jumamosi, 6 Julai 2013

DIC ROBERT MANUMBA AWASHUKURU WANANCHI KWA UTULIVU ZIARA YA BARACK OBAMA

8E9U8650Mkurungenzi wa makosa ya jinai  wa jeshi la polisi nchini Tanzania  DCI ROBERT  MANUMBA  amewashukuru  wananchi  kwa kuonesha  utulivu  na amani wakati  wa ziara ya Rais Baraka Obama  hapa nchini amesma hayo mwakati akizungumza na wandishi wa habari  makao makuu ya jeshi la polisi jijini Dar  es  salaam  leo
Aidha katika mkutano huo na waandishi wa habari   Manumba amesema   pia jeshi la polisi nchini limefanikiwa kukamata meno ya tembo  mia  tatu na  arobaini na moja  maeneo ya kimala jijini dsm  baada ya  jeshi la polisi kufanya upelelezi dhidi ya majangili wa tembo  hapa nchini 
Pia katika taarifa yake kwa waandishi wa wahabari  dci  manumba  ameeleza pia kuwa  jeshi la polisi linamshikili  raia mmoja wa uingereza  kwa tuhuma za kigaidi hapa nchini mala baada ya jeshi lapolisi kumkamata mtu huyo akiwa katika safari  mpaka wa kuvuka kwenda nchini Malawi toka nchini Tanzania,
  Manumba amefanuna kwamba mtuhuyo alikutwa na pasi mbili za kusafilia za Tanzania na Uingereza  ambazo sio harari na zimebainika kuwa nimiongoni mwa pasi zilizo potea katika idara ya uamiaji hapa nchini.
  Pia  Dci amesema mala baada ya jeshi la polisi kupeleleza  limebaini kuwa mtu huyo ni raia wa uingereza  na alikuwa akitafutwa na  serikali ya uingereza kwa tuhuma mbalimbali za kigaidi  mtuhuyo mwenye asili ya  kiarabu  na  anauraia wa Tanzania na uingereza. pia munumba amemewahadhalisha wananchi dhidi ya vitendo vya kigaidi  na kusema kuwa bado  vikundi vya kigaidi  vipo na vinafanya matukio ya kihalifu hapa nchini na AFRIKA MASHARIKI  NA DUNIA NZIMA Pia alitaja mitandao hiyo kuwa ni  mtandao wa alshaababu , bokoharamu na alquider  kuwa vikundi hivyo bado nihatari kwa taifa letu na afrika mashariki  na dunia nzima kwa ujumla  wake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...