Ijumaa, 23 Agosti 2013

MWENGE WA UHURU WAMALIZA ZIARA YAKE DODOMA NA KUANZA ZIARA MOROGORO


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh Dk Rehema Nchimbi Akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Joel Bendera leo.Mwenge wa Uhuru Umemaliza Ziara Yake Mkoani Dodoma na Umeingia Mkoani Morogoro kwa ziara ya siku saba ambapo utazindua Miradi ya Maendeleo Itakayogharimu Shilingi Bilion 8.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Joel Bendera Akiwa Na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro Mh Innocent Kalogeris wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Leo Asubuhi Wilaya ya Gairo Morogoro
Mkuu wa Mkoa Wa Dodoma Mh Dk Rehema Nchimbi Aliyevaa Nguo za rangi za Bluu kutoka kulia akiwa na viongozi wa Mbio za Mwenge  pamoja wananchi wa mkoa wa dodoma jana Asubuhi wakati  wa makabidhiano wa mwenge wa uhuru Mpakani mwa Mkoa wa Dodoma na Morogoro
Mkuu wa Mkoa Wa Dodoma Mh Dk Rehema Nchimbi akiwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Ndugu Juma Ally Simai wakati wa makabidhiano wa Mwenge wa uhuru uliomaliza Ziara Yake Mkoani Dodoma  na kuanza ziara katika Mkoa wa Morogoro.Makabidhiano Hayo yalifanyika Mpakani mwa mkoa wa Dodoma na Morogoro katika wilaya ya Gairo 
Picha


Meya wa manispaa ya Morogoro Mh Juma amir Nondo akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh Antony Mtaka
Viongozi wa serikali na wachama wa mkoa wa Morogoro wakiwa katika makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru jana Asubuhi.
Mkuu wa wilaya ya Bahi Mh Betty Mkwasa akiwa katika tukio Hilo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...