Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa kata ya Iniho Wilayani Makete wakati alipotembelea kata hiyo katika ziara yake ya mkoa wa Njombe leo, Kinana yuko mkoani Njombe kwa ajili ya shughuli za kuimarisha chama na kukagua miradi ya maendeleo katika kusimamia serikali ili kutekeleza ilani ya chama hicho na kuwahimiza wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo.PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MAKETE
Naibu Waziri wa Maji na mbunge wa jimbo la Makete Injinia , Dk. Bilinith Mahenge akiwahutubia wananchi wa kata ya Iniho wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata hio wakati Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana alipotembelea kata hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Makete Bi. Josephine Matiro akizungumza na wananchi kuelezea jinsi serikali inavyotekeleza miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo.Wananchi wa Kata ya Iniho wakiwa katika mkutano huo
Kikundi cha ngoma kikicheza ngoma ya asili ya kinyakyusa inayoitwa Ing’oma.
Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akiteta jambo na Mzee Pascal Sangamjumbe wa shina la Singida katika kata ya Tandala Wilayani Makete wakati katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana alipotembelea katika kata hiyo leo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza na wanachama wa chama cha mapinduazi katika shina la Singida kata ya Tandala wakati alipotembelea katika kata hiyo leo
Mzee Pascal Sanga Mwenyekiti wa shina la Posta katika kata ya Tandala Wilayani Makete akifungua kikao hicho baada ya Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na ujumbe wake kutembelea tawi hilo.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na ujumbe wake akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Makete Bi. Josephine Matiro kutembelea tawi la Singida kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Makete Francis Chaula
Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia wananchi katika kata ya Iniho Wilayani Makete.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni