Jumapili, 1 Desemba 2013

ABOOD AHIMIZA MAFUNZO YA MIRADI KWA WANAWAKE.

MBUNGE wa jimbo la Morogoro mjini Aziz Abood amewataka wanawake kuhakikisha wanabuni miradi iliokuwa na  soko sambamba na kupata mafunzo kabla ya kutekeleza miradi hiyo ili iweze kuwa na tija.
Abood alisema hayo jana wakati alipokuwa akifungua baraza la jumuiya ya wanawake wa chama cha Mapinduzi CCm mkoa wa Morogoro.
Alisema kuwa ni vema kabla wanawake hao hawajaanzisha miradi yao wawe wamepata mfunzo ya ujasiliamali ili kuweza kuendesha kwa ufanisi bila kuingia hasara.
‘’ Wanawake wanaposhirikishwa katika masuala ya ujasiliamali ni muhimu kupatiwa elimu kwanza, hii itasaidia kuweza kuendesha miradi yao kwa faida’’ Alisema
Aidha Abood aliwataka wanawake hao kujiunga katika vikundi mbalimbali ili kuweza kujihusisha na masuala ya kilimo na ufugaji miradi ambayo ni rahisi kutekelezeka na kwamba ina soko la uhakika.
Kwa upande mwingine mbunge huyo aliwataka UWT mkoa wa Morogoro kuhakikisha wanafika kwa wanachama wao kuanzia ngazi za chini ili  kusikiliza kero za wanachama wake  badala ya kukaa ofisini na kuongeza kuwa chama kisichotoka na kuangalia kero za wanacama wake ni chama cha viongozi.
Pia aliwahimiza kuhakikisha wanaongeza wanachama wengi zaidi katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa ili chama hicho kiweze kuendelea kushika dola kwa uhakika zaidi.
Vile vile aliwataka madiwani kuhakikisha wanagomea miradi ya maendeleo katika kata zao ambayo iko chini ya viwangi .
Naye katibu wa UWT mkoa wa Morogoro Tuhuma Lihepa Alisema kuwa wameanda mkakati wa kuwa na miradi ya kilimo na ufugaji nyuki  ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuondoakana na dhana ya kuombauomba  katika kuendesha shughuli za jumuiya hiyo.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Morogoro Mariam Kiamani alisema kuwa jumuiya hiyo mkoani hapa iko imara  na kwamba kamwe hawatayumbishwa na wapinzani.
Alisema kuwa UWT imejiimarisha katika ngazi zote na kwamba kamwe hawawezi kuyumbishwa na vyama ambavyo havina sera wa dira na kwamba anachofanya kwa sasa ni kuhakikisha jumuiya hiyo wanavunja makundi yote ya uchaguzi ili kuweza kujiimarisha zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...