Ijumaa, 21 Februari 2014

MTAKA AMSHUKURU MEMBE KWA KUFADHIRI WANARIADHA 40 KWENDA CHINA, URURUKI NA ETHIOPIA KWA MAFUNZO YA RIADHA.

 



RAIS wa shirikisho la riadha Tanzania RT  Antoni Mtaka  amemshukuru waziri wa mambo ya nje Bernard Membe kwa kufadhili wanariadha 40 kwenda nchi za China Uturuki na Kenya kwaajili ya mafunzo.
Mtaka ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Mvomero alisema hayo Februari 21 mwaka huu wakati akiongea na waandishi wa habari mjini hapa.
Alisema kuwa mafunzo hayo ni maandalizi ya mashindano ya jumuiya ya Madola yanayotarajiwa kufanyika mwezi Julai mwaka huu nchini Glassgon nchini Scotland.
Alisema kuwa wanariadha 20kati ya hao watakwenda nchini China,  wengine 10 watakuwa nchini Uturuki,  na 10 watakwenda nchini Ethiopia  sambamba na makocha 6 ambao nao wanakwenda kupata uzoefu.
Alisema kuwa wanariadha 2 watakwenda nchini Kenya kwa ofa ya waziri wa habari utamaduni na michezo Finela Mkangala ambaye alitoa ofa hiyo wakati wa mbio za kifimbo cha malkia Elizabeth.
Alisema kuwa wanariadha wengine 35 watakuwepo hapa nchini katika mikoa ya Dodoma na Manyara ambao watachujwa na hao watakaotoka nje na kwenda katika mashindano hayo ya jumuiya ya Madola.
Alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuboresha mchezo huo na kuweza kuleta ushindi hapa nchini badala ya kubakia kuwa kama washiriki au watalii kama ilivyokuwa hapo awali.
‘’ Hatutaki kubakia kama watalii au washiriki sasa, tunataka kuwa washindi, watakaokwenda ni wale tu wanaokidhi vigezo’’ Alisema
Pia Mtaka alitoa wito kwa wadau na viongozi mbalimbali kuiga mfano huo kwa kuwasaidia wanariadha hapa nchini ili kukuza mchezo huo.
Alisema kuwa mbio hizo zitakazoshindaniwa ni pamoja na mbio fupi, mbio za kati na mbio ndefu sambamba na marathon , miruko na mitupo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...