Alhamisi, 3 Julai 2014

FEDHA ZA RADA ZAMWAGA MADAWATI YA PLASTIKI MORO.

Naibu meya wa manispaa ya Morogoro Lidya Mbiaji akikabidhi dawati kwa mkuu wa shule ya msingi Bungo Roman Luoga huku  kaimu afisa elimu wa manispaa ya Morogoro   Christopher Wangwe akishuhudia.
 Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro akiwa katika picha ya pamoja na waratibu wa elimu kata, baada ya kukabidhi madawati ya Plastiki yaliotokana na fidia ya fedha za Rada.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Mazimbu B wakifungua maboksi ya madawati hayo .




HALMASHAURI ya  Manispaa ya Morogoro imepokea madawati 756 kutoka Serikali kuu yalionunuliwa kwa fedha za fidia ya Rada.

Madawati hayo aligawiwa jana katika shule 9 za manispaa  hiyo sambamba na vitabu 127,867 vya masomo yanayofundishwa shule za msingi.

Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro Lidya Mbiaji alisema hayo jana wakati akikabidhi madawati hayo kwa walimu wakuu wa shule hizo.

Aliwataka wazazi na walezi wa watoto hao kuwajibika katika kuyatunza madawati hayo ili yaweze kudumu na kuondokana na kero ya madawati.

Hata hivyo aliwataka walimu wakuu wa shule zilizopatiwa madawati hayo kuhakikisha wanatoa madawati hayo kwa wanafunzi ambao wenye kuweza kuyatunza .

Kaimu mkurugenzi wa Manispaa hiyo Philemon Magesa alisema madawati hayo yamekuja wakati manispaa hiyo ikiwa na upungufu wa madawati takribani 7000.

 Alisema pamoja na kupata madawati hayo  sio kigezo kwa wazazi na walezi kubweteka katika zoezi la kuchangia suala zima la madawati.

Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii Zumo Makame alisema msaada huo utasaidia kuondoa kero kwa wanafunzi ambao walikuwa wakikaa chini kwa kukosa madawati wakati wa kusoma.

Alisema kamati ya huduma za jamii inalenga kuboresha elimu na hivyo kuhakikisha wanaondoa kero zote zinazokabili elimu ili kutoa fulsa kwa wanafunzi kufanya vizuri katika masomo yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...