Jumanne, 19 Novemba 2013

CHAMA cha Mapinduzi CCM mkoa wa Morogoro kimeagiza kata ya Kibaoni kuitisha  mkutano mkuu wa halamashauri kuu ya kata ya Kibaoni iliopo wilayani Kilombero ili kumjadili katibu kata wa CCM wa kata hiyo kwa tuhuma za ulevi.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Morogoro Innocent Kalogiries Alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza katika mkutano mkuu wa halimashauri ya kata hiyo.
Alisema alilazimika kutoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wajumbe wa Halmashauri kuu ya kata hiyo kuwa katibu wa kata hiyo John Uwaya  alikuwa amekithiri kwa vitendo vya ulevi na hivyo kushindwa kutimiza majukumu yake ya kazi.
‘’ Hili lipo ndani ya uwezo wenu, itisheni mkutano wa halmashauri kuu ambao ndio uliomchagua, muende na ajenda ya kumsimamisha kisha kumwondoa . Alisema.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa imefika wakati kwa sasa viongozi wasiofaa ni vema wakaenguliwa kama wenyewe hawataki kujiengua ili kunusuru chama.
Hata hivyo mwenyekiti huyo aliwataka viongozi wa wanachama wa CCM kuwa hakuna chama madhubuti kama CCM na kwamba wasijaribu kushawishika na vyama vingine kwani amani na utulivu wan chi utatoweka.

‘’ Mtakaoumia ni nyie na watoto wetu, hao mnaowaona wanahangaika na vyama vya upinzani ikitokea kuvunjika amani wanauwezo wa kukimbilia nchi nyingine’’ Alisema.

Alisema kuwa yapo mataifa ambayo yalijaribu kubadilisha chama kwa lengo la kudhani watapata manufa na badala yake wakaambulia vita.
Kwa upande wao wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM kata ya Kibaoni waliomba CCM wilaya hiyo kutowaingilia na kubeba wagombea wao wa udiwani katika uchaguzi mdogo na badala yake wawaachie wachague mtu ambaye wao wanaona anawafaa.
‘’ wilaya tunaomba ituachie kata katika uchaguzi huu wenyewe, wapo viongozi ambao tayari wameanza kuja’’ alisema Said Tomas Lupia.
Kata ya kibaoni ipo katika mchakato wa kutafuta diwani baada ya diwani wa kata hiyo Salumu Msika kufariki dunia mapema mwezi juni mwaka huu
Mwisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...