Jumapili, 24 Novemba 2013

DC Kilombero alalamikiwa kuvunja Serikali za vitongiji

MKUU wa wilaya ya Kilombero Hasani Masala amelalamikiwa kwa kitendo cha kuvunja uongozi katika serikali za vitongoji vitatu  katika kijiji cha Mkangawalo  kata Mngeta  wilaya Kilombero mkoani Morogoro na kusimika viongozi wengine.

Malalamiko hayo yametolewa jana  na wananchi wa kata hiyo ya Mngeta wakati wa ziara ya katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Morogoro wilayani Kilombero.

Wananchi hao walisema kuwa mkuu wa wilaya huyo alivunja serikali hizo Mei 23, 2013  baada ya kufika kijijini hapo na kudai kuwa viongozi wa serikali hizo wanatuhumiwa kwa ubadhirifu wa fedha na kwamba wanatakiwa kusimamaishwa ili uchunguzi ufanyike.

Mkuu huyo wa wilaya alipofika kijijini hapo alivunja serikali za vitongoji vya Itongoa A, Itongoa B na Mgudeni kwa madai kuwa viongozi wake wanatuhumiwa kwa ubadhilifu wa  fedha.

Mmoja  wa wanachi hao  Richard Mwamwanga alisema  mkuu wa wilaya huyo alipofika kijijini hapo alivunja uongozi huo kwa madai kuwa uchunguzi hauwezi kufanyika wakati viongozi hao wakiwa madarakani na aliahidi kupeleka mrejeho wa uchunguzi huo.

‘’ Chakushangaza ni kwamba baada ya wiki moja, Mei 30, 2013 uchaguzi ulifanyika na hadi sasa miezi sita imepita DC huyu hajaleta mrejesho wowote’’ Alisema.

Hata hivyo alisema kuwa awali wananchi hao walipomuuliza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero Hazimina Mbilinyi alidai kuwa utaratibu uliofanywa na mkuu huyo wa wilaya sio sahihi na kwamba atachukua hatua.

‘’Baada ya muda mkurugenzi huyo alifika tena na kuwasimika viongozi hao jambo ambalo liliwachanganya wananchi hao’’ Alisema Mwamwanga.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero David Ligazio alisema kuwa baada ya  kutokea tatizo hilo alimwagiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo kumshauri mkuu wa wilaya hiyo juu ya sheria husika za Tamisemi kwa kuwa uongozi huo umechaguliwa kisheria na kwamba vinatakiwa kuvunjwa kisheria.

Alisema kuwa yeye kama msimamizi mkuu wa halamshauri hiyo hatambui uongozi huo uliowekwa na mkuu wa wilaya kinyume na taratibu  na kwamba amewaagiza mkurugenzi kufika katika kijiji hicho na kutoa tamko hilo la halmashauri.

Alisema kuwa kutokana na mgogoro huo hadi sasa halmashauri hiyo imesitisha kutoa posho kwa viongozi hao wa pande hizo mbili hadi sheria itakapofuata mkondo wake.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya huyo Hasan Masala alikiri kusimamisha kwa serikali hiyo kutokana na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikiwakabiri viongozi hao na kusema kuwa kama uchaguzi ulifanyika yeye hajui.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...