Jumanne, 19 Novemba 2013

MWENYEKITI wa chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Morogoro Inocent Kalogeris  ameagiza kutohamishwa  watendaji katika ngazi mbalimbali hadi mikutano mikuu na  halimashauri za CCM katika  ngazi husika zikae na  kusomewa mapato na matumizi.

Mwenyekiti huyo alisema hayo jana wakati akizungumza katika kikao cha halimashauri kuu ya CCM kata ya Kibaoni wilayani Kilombero mkoani hapa.
Alisema kuwa  mtendaji yeyote asiruhusiwe kuondoaka katika eneo lake la kazi bila kusoma mapato na matumizi na kujua kama hakuna ubadhilifu wa aina yeyote.
‘’ Sio kwa watendaji tu bali hata viongozi wa kuchaguliwa, hakuna kujiuzuru  hadi wanachama wajue mapato yao’’ Alisema.
Alisema kuwa kumekuwa na tabia kwa baadhi ya watendaji wasio waadilifu kufanya ubadhilifu sehemu moja na kuhamishiwa sehemu nyingine jambo ambalo alisema linaendelea kukiumiza chama cha Mapinduzi.
Aidha aliwataka viongozi kila mmoja kutimiza wajibu wake katika eneo lake badala ya kutegemea viongozi wa ngazi za juu kuwatatulia matatizo yao.
 
Hata hivyo alisema kuwa kwa sasa umefika wakati wa kuweka viongozi wenye maadili ambao wanaweza kukiongoza chama na sio kuchagua viongozi wanaotoa rushwa.
 ‘’ Tusipoikataa rushwa chama tunakiua, tunapotea ndugu zangu, fedha unayopewa inakuhukumu kwa kipindi chote cha uongozi  uliomchagua’’ Alisema.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa CCM mkoa wa Morogoro kamwe hautavumilia kuona viongozi wanaogombea na kwamba watakaobainika kuwa na hila kama hiyo na kwamba  watachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kuwaengua katika nafasi zao.
mwisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...