Ijumaa, 7 Juni 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILLAL AONGOZA KILELE CHA SIKU YA MAZINGIRA KITAIFA NAMANYERE MKOANI RUKWA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akihutubia wananchi katika viwanja vya sabasaba Mji mdogo wa Namanyere Mkoani Rukwa katika kuhitimisha siku ya mazingira duniani ambayo kitaifa imefanyika Mkoani Rukwa jana tarehe 05.06.2013. Katika hotuba yake hiyo alisisitizia juu ya uhifadhi wa mazingira kwa kutunza vyanzo vya maji, milima na misitu ya asili, kuhifadhi ardhi na kupanda miti katika maeneo yaliyoathirika na usafi wa mazingira kwa ujumla.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akikagua kitalu cha miche ya miti mbalimbali ya mjasriamali ndugu Kidevu (kushoto) katika maonyesho kwenye kilele cha siku ya mazingira kitaifa Mkoani Rukwa katika Mji mdogo wa Namanyere wilayani Nkasi jana tarehe 05.06.2013, Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Terezya Luoga Huvisa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...