Jumatatu, 21 Aprili 2014

DC MVOMERO AWAJIA JUU WANAOWATUKANA WAASISI WA NCHI

 Mkuu wa wilaya ya Mvomero Antoni Mtaka akiongea na umoja wa  wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo vikuu wenye imani ya Kipentekoste wakati wa mahafari ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya sekondari na vyuo ( TAYOMI)iliofanyika melela wilayani Mvomero.
 Mkuu huyo wa Wilaya akimtunuku cheti mwanafunzi wa chuo kikuu cha mzumbe Caroline Ndosi katika mahafari hayo ya kidini.
 Wanafunzi hao wakisikiliza kwa makini hotuba ya mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mtaka.
Wanafunzi hao wakiwa katika picha ya pamoja na DC huyo
Habari zaidi
soma hapa chini
MKUU wa wilaya ya Mvomero Antoni Mtaka amewatahadharisha vijana  wasomi kutoruhusu kukanyaga historia ya waasisi wa Nchi  kwani waliweza kufanya mambo makubwa na wanatakiwa kuenziwa.
Alisema hayo jana wakati akiongea  katika kongamano  la umoja wa wanafunzi walioko shuel za msingi, sekondari na vyuo vya kati  na vyuo vikuu walio na msingi wa imani ya Kipentekoste  (TAYOMI) iliofanyika  Milela wilayani Mvomero.
Alisema wapo baadhi ya watu ambao wamefilisika kimawazo na fikra wanatumia muda wao mwingi kujadili na kutukana mambo waliofanya waasisi hao badala ya kujadili masuala ya katiba yaliopo sasa.
‘’ Unakuta wapo watu wanadiliriki kumtukana Nyerere bila kujali kuwa ndiye aliyetuletea uhuru wan chi hii, nchi nyingi za  Afrika zimekuwa zikimuenzi Nyerere  kwa kutambua mchango wake katika kupatikana kwa uhuru wan chi zao’’ Alisema
Alisema kama nchi  hizo zinatambua umuhimu wake na kumuenzi inashangaza na watangaaa kuona watanzania hawathamini mchango wake na badala yake wanamtukana.
Alisema Nyerere na waasisi wengi wan chi hii walifanya mambo makubwa sana nay a kihistoria hivyo kwa vijana wanayo kila sababu ya kuyaenzi kwa heshima zote na kuwapuuza watu hao wanaobeza mchango wao viongozi hao.
Mkuu huyo wa wilaya aliwataka vija hao wasomi kutumia muda mwingi kufutilia suala zima la mchakato wa katiba na kupembua vipengele muhimu ili ikifika wakati wa kupiga kura iwe rahisi kwao .
‘’ Watu wengi wamejipatia umaarufu kupitia katiba mpya wakidhani katiba ile inaishia bungeni tuu, kumbe katiba ile mchakato wake itarudi tena kwa wananchi na kupigiwa kura’’ Alisema
Kwa upande wake Philipo Abiud Mratibu wa TAYOMI wa mkoa wa Morogoro alisema wamekuwa na utaratibu wa kufanya makongamano kama hayo wakati wa sherehe za Pasaka kwa kuwakusanya  wanafunzi hao na kuwafundisha masuala mbalimbali ya maadili.
Alisema suala kubwa wanalosisitiza ni kujiepusha na madawa ya kulevya kwa vijana hao sambamba na tabia zote zinazopelekea kutumbukia katika vitendo viovu na kuongeza kuwa wanawafundisha kufanya juhudi na maarifa wakiwa shuleni ni waweze kufanikiwa katika maisha yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...