Ijumaa, 11 Julai 2014

GARI LA MAKAL LAENDELA KUSHIKILIWA NA TRA.

     Gari lenye namba za usajiri T  534 BFP Toyota Dyna linalomilikiwa na  Gabriel Amos makal , linaendelea kushikiliwa na mamlaka ya mapato Tanzania mbali na gari hilo kulipiwa deni la sh 662,500 iliokuwa ikidaiwa kama ushuru wa barabara.



Namba ya simu inayodaiwa kutuma ujumbe wa vitisho kwa TRA hiyo hapo.  0763 444455  baada ya gari hilo kukamatwa. 
Ujumbe wa kwanza ''silipi,''
Ujumbe mwingine huu aliotuma ni  ‘’  mazingira ya kukamata hilo gari  ni ya kihuni na ii inaonyesha namna gani ht raia wa kawaida wanavyopata taabu watu hawana vitambulisho, wamewashurutisha  wangu, nabaki na msimamo kuwa zoezi mnalolifanya na kero ninazopokea toka kwa wananchi kuwa TRA Mvomero ni wakatili na wananyanyasa wananchi ss mimi mwakilishi  wa wananchi nimethibitisha, kwa vitendo  najua hatua za kuchukua kny ya wananchi wangu’’ 

TAARIFA ZAIDI ZITAWAJIA HIVI PUNDE.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...