Ijumaa, 7 Juni 2013

MAMA SALMA KIKWETE ATEMBELEA KITUO CHA KUREKEBISHA TABIA KWA WANAWAKE NA WASICHANA WATUKUTU CHA PERTAPIS HUKO SINGAPORE.

IMG_5786Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Mama Salma Kikwete akipokea ua kutoka kwa msichana anayetunzwa katika kituo cha watoto wa kike watukutu cha Pertapis kilichoko Singapore wakati alipokitembelea kituo hicho tarehe 6.6.2013. Mama Salma yupo nchini Singapore akiambatana na Rais Kikwete katika ziara ya kikazi ya siku mbili nchini humo. Kulia ni Mkuu wa kituo hicho Mama Sahnim Sokaimi.IMG_5796Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika mazungumzo rasmi na uongozi wa kituo cha kuwatunza wasichana na wanawake watukutu cha Pertapis kilichoko nchini Singapore.IMG_5840Mwenyekiti wa WAMA na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisisitiza jambo wakati wa kikao cha pamoja kati yake na uongozi wa kituo cha kuwarekebisha tabia wanawake na wasichana cha Pertapis kilichoko huko Singapore wakati alipokitembelea tarehe 6.6.2013. Kushoto kwa Mama Salma ni Mama Badriya Kiondo, Afisa kutoka ubalozi wa Tanzania nchini India. IMG_5884Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa somo kwa wasichana watukutu wanaotunzwa kwenye kituo cha kurekebisha tabia zao cha Pertapis kilichoko jijini Singapore wakati alipokitembelea tarehe 6.6.2013.
IMG_5892IMG_5916Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akizungumza na Mama Sahnim Sokaimi, Mkuu wa kituo cha kurekebisha tabia za wanawake na wasichana watukutu cha Pertapis kilichoko nchini Singapore mara baada ya kukitembelea tarehe 6.6.2013.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...