Jumanne, 21 Januari 2014

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDAMAFUNGA MAFUNZO KWA VIJANA KUHUSU UTENGENEZAJI WA MATOFALI LEO

pm1..Waziri Mkuu Mhe. Mizonge Pinda akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Nehemia Mchechu mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya ufungaji wa mafunzo kwa Vijana waliowezesha kupata taaluma ya utengenezaji wa matofali kwa teknolojia ya kisasa. leo jijini Dar es Salaam.pm1Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungana wa Tanzania Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sihaba Nkinga wakati alipo wasili katika hafla ya ufungaji wa mafunzo kwa vijana kuhusu utengenezaji wa matofali leo jijini Dar es Salaam.pm2Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara akimkaribisha Waziri Mkuu ali aweze kuzungumza na Vijana wahitimu wa mafunzo ya ujenzi wa matofali kwa teknolojia ya kisasa na gharama nafuu leo jijini Dar es Salaam. Mafunzo hayoyamenedeshwa na  Wakala wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi(NHBRA), kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na na kushirikisha idadi ya washiriki 50 kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini.pm3Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungana wa Tanzania Mizengo Pinda akihutubia wahitimu pamoja na wageni waalikwa katika hafla ya ufungaji wa mafunzo kwa vijana kuhusu utengenezaji wa matofali kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu iliyofanyika katika ofisi za Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA) leo jijini Dar es Salaam.

pm4.aziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungana wa Tanzania Mizengo Pinda akiangalia baadhi ya Matofali ambayo tayari yamekwisha tengeznezwa kwakutumia teknolojia waliyofundishwa wahitimu hao leo jijini Dar es Salaam kushoto ni Waziri wa  Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella  Mukangara.
pm5Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya Ufundi wa utengenezaji Natofali kwakutumia teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu wakimsikiliza Waziri Mkuu(hayupo pichana) wakati akiwahutubia kwenye hafla ya kufunga mafunzo yao na kuwakabidhi vyeti.
Picha zote na Frank Shija – Wizara ya Habari

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...