Jumapili, 25 Mei 2014

CCM MORO YAKUSUDIA KUWABURUZA MAHAKAMANI WAPANGAJI WAO WENYE MADENI SUGU

CHAMA cha Mapinduzi CCM mkoa wa Morogoro kimesema kitawachukulia hatua  za kisheria kwa kuwafikisha mahakamani  wapangaji wake wote ambao wanamadeni sugu  sambamba na kupitia upya mikataba kuona kama iko sahihi.

Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Rojas Romuli alisema hayo jana wakati akiongea na Uhuru ofisini kwake  ambapo alisema kazi hiyo ni utekelezaji wa maagizo ya baraza la wadhamini.

‘’ Tumeanza kufutilia wapangaji wetu wote wenye madeni sugu ili waweze kulipa , vinginevyo watakaokaidi tutawachukulia hatua za kisheria’’ Alisema

Romuli alisema hatua za kisheria watakazochukua ni pamoja na kuwafungia biashara zao  na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

Alisema pia wanafanya mapitio ya kodi za wapangaji wao kuona kama zinalingana na mazingira na wakati sahihi kwa lengo la kuhakikisha miradi hiyo inakuwa na tija kwa chama.

Aidha alisema  wakati huo huo wanapitia mikataba ya wapangaji wao kuona kama iko sahihi na kwamba wale wote ambao hawana mikataba kuwataka kujaza mikataba ili kuweza kufanya kazi nao.

‘’ Wapo baadhi ya wapangaji wetu ambao hadi sasa hawana mikataba, kwa sasa ni lazima kila mpangaji akawa na mkataba’’ Alisema

Hata hivyo alisema  lengo la kufanya hivyo ni pamoja na kuhakikisha wanaiboresha miradi hiyo ili iweze kukidhi mahitaji ya sasa kulingana na eneo husika.

Alisema Kwa sasa walianza kufanya ukarabati katika jengo la ofisi  ya CCM mkoa na kwamba  kila ilipo miradi yao itaboreshwa ili ilingane na mazingira halisi .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...