Jumapili, 25 Mei 2014

MANISPAA MORO YAFUNGA GEST 54 ZINAZOENDESHWA BILA LESENI



HALMASHAURI ya manispaa ya Morogoro imefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi milioni 50  kwa wafanyabaishara walikokuwa wakiendesha biashara zao bila leseni.
Afisa habari wa manispaa hiyo Liliani Henerico  alisema hayo jana wakati akitoa taarifa ya oparesheni ilioendeshwa na mansiapaa hiyo katika nyumba za  kulala wageni na maduka mjini hapa.

Alisema oparesheni hiyo ilifanywa katika kipindi cha mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu na kwamba jumla ya biashara 54 zilifugiwa kutokana na kushindwa kulipa faini hizo.
Alisema katika zoezi hilo faini za leseni zilikuwa ni shilingi 4,540,000 ambapo  mapato ya ada za leseni yalikuwa ni 45,786859 n hivyo kufanya jumla ya makusanyo hayo kuwa ni shilingi milioni 50,326,859.

 Aidha afisa habari huyo alisema zoezi hilo linaendelea kuhakikisha wafanyabiashara wote wanafata taratibu na kuepuka kukwepa kodi.

Kwa upande mwingine afisa habari huyo alisema manispaa hiyo ilianza zoezi la kukagua nyumba katika manipaa hiyo kuhakikisha mazingira  yanakuwa safi na salama.

Alisema utekelezaji wa zoezi hilo la usafi wa mazingira hadi sehemu za makazi ya wananchi ni agizo la mkuu wa mkoa la kutaka halmashauri zote kuhakikisha zinakuwa safi ili mkoa wa Morogoro uweze kupata tunzo ya usafi kitaifa.

Sambamba na hilo alisema agizo hilo pia ni kutaka kujenga mazingira ya kuepuka maradhi ya mlipoko kwa wakazi wa  mkoa wa Morogoro

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...