Ijumaa, 23 Mei 2014

MZUMBE WATAKA MITANDAO YA KIJAMII ITUMIKE KUJIFUNZIA SIO BURUDANI PEKEE





WANAFUNZI  wa vyuo  vikuu wametakiwa kutumia mitandao ya kijamii kwaajili ya  kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu masomo yao badala ya kutumia kwa kujifurahisha kama ambavyo wengi wamekuwa wakifanya hivyo.
 Hayo yalisemwa jana na  naibu  makamu  wa mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe Profesa Josephat  Itika wakati wa kongamano la wanafunzi wanaosoma masomo ya uhasibu chuoni hapo.
 
Alisema mara nyingi wanafunzi hao wamekuwa wakitumia mitandao hiyo kwa kujiburudisha na kwamba  mitandao hiyo ingekuwa na manufaa kwao kama wangetumia kupata vitu vinavyowasaidia katika masomo yao.
“ Katika mitandao kuna fulsa nyingi za elimu, watumie fulsa hizo kuendeleza fani zao, wapunguze muda wa kuchati na meseji za kujifurahisha tu’’ Alisema.
Hata hivyo  alisema  katika kongamano hilo wanafunzi walipata fulsa ya kukutana na wataalamu mbalimbali  wa masuala yanayohusu uhasibu na kuweza kubadilisha uzoefu kwa lengo la kwenda na wakati.
Aidha alisema moja ya changamoto inayowakabili wasomi ni soko la ajira ambalo hubadilika kila siku hivyo ni lazima kuhakikisha wanakidhi mahitaji hayo.
‘’ Sisi kama waadhiri tunachofanya ni kufanya utafiti kila wakati na kujua nini kinahitajika katika soko la ajira na ndipo tunakuja kuwaletea wanafunzi wetu, sio kukazania kusoma vitabu tuu’’ Alisema.
Naye Hawa Tundui muhadhiri katika chuo hicho alisema kwa sasa wahitimu ni wengi hivyo soko la ajira  ni gumu ukilinganisha na miaka ya 1980 hivyo ni lazima kwa vyuo huria vikaangaia jinsi gani ya kuwafundisha wanafunzi wao kulingana na soko la ajira.
Alisema kongamano hilo linawabadilisha mtazamo wanafunzi hao kujua mbinu mbadala za kuweza kujiajiri badala ya kubakia na mtazamo wa kupata ajira.

Husen Maneno  mwanafunzi wa mwaka wa pili anayechukua masomo ya biashara katika chuo hicho alidai kumekuwa na ucheleweshaji wa kubadili mitala kwenda na wakati  hapa nchini na kwamba hiyo ni changamoto kubwa inayowakabili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...