Jumapili, 10 Agosti 2014

KOMBANI ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VIFUFULIWE

. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Celina Kombani amewataka wakulima kusahau yaliopita juu ya vyama vya ushirika na kuvifufua kwani ndio mkombozi wao, Alisema hayo wakati wa kuhitimisha kilele cha siku ya wakulima 88 mkoani Morogoro.
 
 Kombani akisindikizwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadiq, pamoja na mwenyekiti wa TASO kanda ya Mashariki Mohamed Mzee ,a katibu wake Rafael kumtunza mwana dada huyo aliyekuwa kivutio cha burudani katika maonyesho hayo baada ya kupiga danadana kwa zaidi ya nusu saa bila mpira kumponyoka.
 Mkuu wa wilaya ya Mvomero Antoni Mtaka akiwa katika moja ya bada linalozalisha mahindi ya lishe lijulikanoalo kama CPP Tanzania Co.LTD, Mtaka ni miongoni mwa wakulima wa mbegu hiyo mkoani Morogoro, baadhi ya wananchi walimwambia Mtaka kwamba ameonyesha kipaji chake kuwa  ni kilimo na kumtaka kuwashawishi viongozi wengine kuiga mfano wake, 
'' Mimi ni mkulima, nimeanza kuonyesha kipaji changu, sio kusubiri hadi ustaafu ndio unaanza kutafuta cha kufanya,'' alisema Mtaka.
 Mahindi yaliotumika kuonyesha mfano katika banda hilo yanatoka katika shamba la Mkuu huyo wa wilaya ya Mvomero Mtaka ambayo amelima wilayani humo.
 Viongozi wa wilaya ya Kilombero wakiwa katika maonyesho hayo siku ya kilele cha 88 mkoani Morogoro.
 Maafande wa JKT kanda ya mashariki wakipokea zawadi ya ushindi wa kampuni za zana za kilimo ambapo wamenyakua nafasi ya kwanza.
 Makamo mkuu wa chuo kikuu cha kilimo SUA Profesa Monella akipokea zawadi baada ya kushika nafasi ya kwanza katika kilimo na utafiti.
 Meya wa Manispaa ya Morogoro akiwa katika maonyesho hayo na viongozi wengine mkoani hapa.
 Msanii kutoka wilaya ya Bagamoyo akionyesha fani yake kwa kuigiza kujikata panga ambalo lilionekana kuingia mwilini pasipo kutokwa na damu.
Wasanii kutoka Mtibwa wakionyesha burudani ya sarakasi kwa kutumia viti vulivyopangwa juu ya chupa za bia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...