Alhamisi, 18 Septemba 2014

WATU WATANO WANASHIKILIWA NA POLISI KWA UJAMBAZI MORO.



Kamanda wa  polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul,  akionyesha moja ya silaha zilizowahi kutumika katika matukio ya uharifu hivi karibuni.




habari zaidi soma hapo chini.


WATU watano wanashikiliwa na polisi mkoani hapa, kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya ujambazi  mkoani Morogoro na Dodoma, akiwemo mwanamke mmoja.

 


Kamanda wa Polisi mkoani hapa Leonard Paul, alisema watu hao walikamatwa  Septemba 17  mwaka huu majira ya mchana huko Kijiji cha Luhembe tafara   ya Mikumi wilayani Kilosa.


Alisema majambazi hayo  yanadaiwa kufanya tukio la ujambazi mkoani Dodoma kisha kukimbilia mkoani Morogoro,ambapo polisi  wa mikoa hiyo miwili ndio walifanikisha kukamatwa kwao.



Alisema  mmoja wa majambazi hao alikamatwa mkoani Dodoma,baada ya kufanya uharifu na kwamba ndiye alifanikisha kukamatwa kwa wenzake baada ya  msako mkali wa polisi.


Hata hivyo kamanda huyo alisema baada ya kuwakamata majambazi hao ,walifanikiwa kukamata bunduki aina ya MSG yenye namba za usajili 380859.


Alisema mbali na bunduki hiyo polisi hao walifanikiwa kukamata meno ya tembo mawili aliokutwa nayo mmoja wa majambazi hao huko Luhembe.


Hata hivyo kamanda huyo alisema polisi wa mikoa hiyo miwili wanaendelea kutafuta silaha na majambazi wengine , waliohusika na tukio hilo na kuwataka wananchi kutoa taarifa za watu wanaowatalia mashaka.
 
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...