Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Bw. Laurence Bay, Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Singapore. Kushoto ni Balozi wa Tanzania India na Singapre Injinia John Kijazi na mbele yao ni Naibu Mkurugenzi wa Itifaki wa Singapore Bi. Christine Tay.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe, Waziri wa Viwanda na Baishara Dk. Abdallah Kigoda na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka mara baada ya kuwasili kwenye hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC ) kilichoenda sambamba na mkutano wa wafanyabiashara wa Singapore ambapo Rais Kikwete aliwakaribisha kuja kuwekeza nchini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Kasulu mjini Mhe Moses Machali pamoja na wadau wengine wakati akiwasili Singapore.
Picha juu na chini ni Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea jijini Singapore leo wakati alipokutana na wafanyabaishara za ujenzi wa nchi hiyo marav tu baada ya kutua kutoka Japan alikokuweko kwa ziara ingine ya kikazi. Katika mkutano huu Rais Kikwete aliwakaribisha wafanyabishara hao wa Singapore Tanzania kuwekeza katika sekta ya nyumba wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).(Picha na IKULU).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni