Ijumaa, 3 Januari 2014

UVCCM YAMFAGILIA KIKWETE KWA MALEZI BORA, NI KATIKA UCHAGUZI MKUU WA CHIPUKIZI MORO

 Mwenyekiti wa umoja wa Vijana Taifa Sadifa Juma Khamis akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa Chipukizi uliofanyika katika shule ya sekondari ya wasichana ya Kilakala mjini Morogoro.
 Mlezi wa chipukizi Taifa Dk Abdala Kigoda Akitoa neno la shukrani baada ya mkutano kufunguliwa.

 Baadhi wa wagombea wa Chipukizi wakisubiri hatma yao.
 Wajumbe wa mkutano mkuu wa chipukizi Taifa wakifutilia mkutano huo kwa makini.

Katibu mkuu wa UVCCM Taifa Sictus Mapunda akiteta jambo na Mlezi wa chipukizi Dk Abdalla Kigoda Nje aya ukumbi mara baada ya mkutano kufunguliwa..


HABARI ZAIDI , SOMA HAPA.

MWENYEKTI wa Umoja wa Vijana Taifa Sadifa Juma Khamis amempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kwa malezi ya kuilea jumuiya hiyo  na kazi kubwa ya kuleta maendeleo ya taifa.
Sadifa alisema hayo jana wakati akifungua mkutano mkuu wa Chipukizi Taifa uliofanyika katika shule ya sekondari ya Kilakala mjini Morogoro.
 
Alisema kuwa chama cha Mapinduzi lina jukumu kubwa la kulea jumuiya zake na kwamba chimbuko la viongozi wazuri linatokana na Chipukizi.
Aliwataka wazazi na walezi kuwalea chipukizi katika maadili mema ili waweze kuwa viongozi bora wanaoandaliwa kwaajili ya miaka ya badae.
Akitolea mfano alisema kuwa viongozi wengi walioko madarakani kwa sasa walipita katika tanuru la chipukizi na Uvccm na kwamba walilelewa katika maadaili mazuri ambayo yamefikisha kuwa viongozi waadilifu.
‘’ Rais Kikwete ni miongoni mwa mjumbe wa baraza la umoja wa vijana waanzilishi na kwamba leo tunamwona ndio kinara wa nchi’’ Alisema
Kwa upande wake mlezi wa Chipukizi taifa Dk Abdala Kigoda aliwataka baada ya uchaguzi huo kumalizika makundi yavunje kwani yanadhoofisha chama.
Hata hivyo alisema kuwa umoja na mshikamano ndio utakaosababisha CCM kushika hatamu milele na kwamba kamwe hawataki kusikia CCM ikiitwa chama cha Upinzani kwani ndio chama pekee kilichopatia uhuru wan chi ya Tanzania.
Naye katibu mkuu wa UVCCM Taifa Sixtus Mapunda alisema kuwa alipokea hoja mbalimbali kutoka kwa makatibu wa hamasa na chipukizi ikiwemo ya kutaka kushiriki mkutano mkuu wa CCM taifa kama wanavyoshiriki makatibu wa Jumuiya hiyo.
Alisema hoja nyingine ni kutaka ajira za kudumu kwa makatibu hao kama walivyo makatibu wa jumuiya jambo ambalo alisema madai yote wamayapokea na kwamba watayafanyia kazi.
Mwisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...